Sikiliza Live
Monday, 1 April 2013
Wahanga wa kuporomoka ghorofa Dar wafikia 34
Idadi ya viwiviwili vya watu waliokufa kwa kuporomokewa na jengo la
ghorofa jijini Dar es Salaam Tanzania imefikia 34 huku shughuli ya
kutafuta maiti nyingine ikiendelea, zikiwa zimepita siku tatu tangu
ilipotokea ajali hiyo. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Mecky Sadiki
amenukuliwa akisema kuwa, miili mingine kumi imepatikana baina ya jana
mchana na leo Alfajiri na hivyo kuifanya idadi ya watu waliopoteza
maisha yao na ambao wamepatikana hadi sasa kufikia 34. Inakadiriwa kuwa
zaidi ya watu 60 mpaka 70 walikuwa katika jengo hilo la ghorofa kumi na
sita lililoporomoka siku ya Ijumaa. Wakati huo huo, Waziri wa Afrika
Mashariki, Samuel Sitta amesema matukio mengi mabaya kama hayo nchini
yamekuwa yakisababishwa na mafisadi wasiojali maisha ya wengine. alitoa
kauli hiyo alipotembelea eneo la ajali kuwapa pole wafiwa waliopoteza
ndugu zao, akisema kama sheria na kanuni za ujenzi zingezingatiwa tukio
hilo lisingetokea. Katika hatua nyingine, Rais Jakaya Kikwete jana
aliwatembelea majeruhi wa ajali hiyo waliolazwa katika Hospitali ya
Taifa Muhimbili ili kuwafariji.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment