Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 4 April 2013

Mafuriko yasababisha maafa makubwa Argentina

                    24,Jumaadal ula,1434Hijiriyah/ April 05,2013Miyladiyah
 Serikali ya Argentina imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa baada ya watu 52 kufariki dunia kufuatia mafuriko yaliyotokea siku mbili zilizopita katika mji wa La Plata, mashariki mwa nchi hiyo. Watu wengine 6 wameripotiwa kufariki dunia katika viunga vya mji mkuu, Buenos Aires hapo jana Jumatano. Rais Cristina Kirchner ametembelea eneo lililokumbwa na mafuriko na kusema kuwa, serikali itatuma misaada inayotakiwa na vilevile itatuma maafisa zaidi wa polisi kulinda mali za watu pindi watakapokuwa wakihamishwa. Gavana wa La Plata amesema wengi wa wahanga wa janga hilo la kimaumbile walifikwa na mauti baada ya magari yao kufunikwa ghafla na maji. Amesema pia baadhi ya watu walifariki dunia baada ya kuangukiwa na nyaya za umeme zilizoshika maji. Takwimu za serikali zinaonyesha kuwa, zaidi ya watu 2000 wameachwa bila makazi kufuatia mkasa kuo.

0 comments:

Post a Comment