24,Jumaadal ula,1434Hijiriyah/ April 05,2013Miyladiyah
Serikali ya Argentina imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa
baada ya watu 52 kufariki dunia kufuatia mafuriko yaliyotokea siku mbili
zilizopita katika mji wa La Plata, mashariki mwa nchi hiyo. Watu
wengine 6 wameripotiwa kufariki dunia katika viunga vya mji mkuu, Buenos
Aires hapo jana Jumatano. Rais Cristina Kirchner ametembelea eneo
lililokumbwa na mafuriko na kusema kuwa, serikali itatuma misaada
inayotakiwa na vilevile itatuma maafisa zaidi wa polisi kulinda mali za
watu pindi watakapokuwa wakihamishwa. Gavana wa La Plata amesema wengi
wa wahanga wa janga hilo la kimaumbile walifikwa na mauti baada ya
magari yao kufunikwa ghafla na maji. Amesema pia baadhi ya watu
walifariki dunia baada ya kuangukiwa na nyaya za umeme zilizoshika maji.
Takwimu za serikali zinaonyesha kuwa, zaidi ya watu 2000 wameachwa bila
makazi kufuatia mkasa kuo.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment