Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 4 April 2013

‘Serikali isitishe nauli mpya’

        


SERIKALI imetakiwa kusitisha zoezi la kupandisha nauli za mabasi na daladala zinazotarajiwa kuanza kutumika Aprili 12, mwaka huu.
Akizungumza na chanzo chetu Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Morogoro, Susan Kiwanga, alisema serikali inapaswa kuwashirikisha wanachi juu ya mipango yake ili kuepusha mabishano.
Akitoa mfano, alisema kuwa kupanda kwa gharama hiyo kutawafanya wanachi hususan asilimia 80 waliopo vijijini kuendelea kuwa fukara na wengine kupoteza maisha kwa kushindwa kumudu gharama za maisha zinazopandishwa na mfumo mzima wa usafirishaji.
“Serikali lazima iandae mazingira mazuri kwa watoa huduma kama kuondoa kodi na ushuru kwenye vipuli na mafuta, na kuboresha barabara, mfano barabara za vijijini,” alisema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jahazi Asilia Mkoa wa Morogoro, Ismail Rashidi, alisema serikali imekuwa ikijichanganya katika kupambanua hali ya uchumi ikidai uchumi unapanda kwa asilimia saba wakati uhalisia wa pato la Mtanzania ni asilimia tatu.
“Kupandishwa kwa gharama hii ni pigo kwa Watanzania wengi hususan wa vijijini kwa kuwa wanategemea zaidi vyombo vya usafiri kuboresha maisha yao kama kusafirisha mazao na kuja mijini kununua mahitaji ya kijamii,” alisema.
"Chanzo Tanzania Daima"

0 comments:

Post a Comment