Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 4 April 2013

Sheria ya kudhibiti wanahabari Burundi yakosolewa

                             24,Jumaadal ula,1434Hijiriyah/ April 05,2013Miyladiyah
 Bunge la Burundi hapo jana Jumatano lilipitisha kwa wingi wa kura sheria inayolenga kudhibiti sekta ya uandishi habari nchini humo. Sheria hiyo inaipa uwezo serikali kumshurutisha mwanahabari kufichua vyanzo vyake vya habari. Pia inapiga marufuku vyombo vya habari kutangaza au kuchapisha habari kuhusu sarafu ya nchi, usalama wa taifa, wizara na idara za ulinzi pamoja na kuikosoa safu ya juu ya uongozi wa nchi hiyo. Siku moja baada ya sheria hiyo kupitishwa, lawama na ukosoaji umejitokeza kutoka kila kona. Mwenyekiti wa chama cha wanahabari nchini Burundi (UBJ), Bw. Alexandre Niyungeko amesema sheria hiyo inakiuka haki muhimu ya kujieleza nchini humo. Ametoa wito kwa bunge kuwahusisha wadau wote katika sekta ya uandishi habari ili papatikane sheria inayokubalika na pande zote husika. Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch kwa upande wake limelaani hatua ya bunge la Burundi ya kupitisha sheria hiyo na kusema kuwa, serikali inajaribu kuficha uozo katika safu za uongozi.

0 comments:

Post a Comment