WAKATI wananchi wakilalamika kupanda kwa nauli, Mwenyekiti wa
Chama cha Wamiliki wa Daladala, Sabri Mabrouk, amesema nauli hiyo bado
ni ndogo.
Mabrouk alitoa kauli hiyo alipozungumza na kituo kimoja cha redio jijini Dar es Salaam jana na kuongeza kuwa wanaolalamika ni wale walioingia jijini huku wakiwa hawana shughuli maalumu za kufanya.
Alisema ugumu wa maisha haukusababishwa na kupanda kwa nauli bali ulikuwepo tangu utawala wa awamu ya kwanza na utaendelea kuwepo katika tawala mbalimbali zijazo.
“Kwa watu tulioishi pamoja katika maisha ya ugumu ugumu nikisema hivyo wananielewa, lakini najua wapo walionufaika kutokana na kuwa na jamaa ambao walikuwa viongozi katika serikali; hao labda ndio wanaweza kushindwa kujua ugumu wa maisha katika nchi hii.
“Pia wananchi wajue kila kitu kizuri kina gharama zake, hivyo ili kuboresha huduma zetu za usafiri ni lazima wananchi wakubali kuchangia kile kinachostahili,” alisema Mabrouk.
Akizungumzia mfumo wa huduma ya usafirishaji jijini kuwa wa kampuni, Mabrouk alisema haukwepiki bali ni muhimu kwa wamiliki wa daladala kutumia fursa hiyo kujiunga na kuanzisha kampuni.
Mabrouk alitoa kauli hiyo alipozungumza na kituo kimoja cha redio jijini Dar es Salaam jana na kuongeza kuwa wanaolalamika ni wale walioingia jijini huku wakiwa hawana shughuli maalumu za kufanya.
Alisema ugumu wa maisha haukusababishwa na kupanda kwa nauli bali ulikuwepo tangu utawala wa awamu ya kwanza na utaendelea kuwepo katika tawala mbalimbali zijazo.
“Kwa watu tulioishi pamoja katika maisha ya ugumu ugumu nikisema hivyo wananielewa, lakini najua wapo walionufaika kutokana na kuwa na jamaa ambao walikuwa viongozi katika serikali; hao labda ndio wanaweza kushindwa kujua ugumu wa maisha katika nchi hii.
“Pia wananchi wajue kila kitu kizuri kina gharama zake, hivyo ili kuboresha huduma zetu za usafiri ni lazima wananchi wakubali kuchangia kile kinachostahili,” alisema Mabrouk.
Akizungumzia mfumo wa huduma ya usafirishaji jijini kuwa wa kampuni, Mabrouk alisema haukwepiki bali ni muhimu kwa wamiliki wa daladala kutumia fursa hiyo kujiunga na kuanzisha kampuni.
0 comments:
Post a Comment