12Jumaadal Aakhir,1434 Hijiriyah/ April 22,2013 Miyladiyah
Waislamu wa mji wa Montrouge nchini Ufaransa wamepanga kufanya
maandamano makubwa ya kulalamikia hatua ya manispaa ya mji huo ya
kupinga kujengwa msikiti mjini humo. Kituo cha habari ya Echo-Montrouge
kimewataka Waislamu wa mji wa Montrouge wa kusini mwa mji mkuu wa
Ufaransa, Paris, kujitokeza kwa wingi kwenye maandamano hayo ili
kulalamikia hatua ya manispaa ya mji huo ya kuzuia kujengwa kituo pekee
cha ibada kwa Waislamu mjini humo. Maandamano hayo yamepangwa kufanyika
wiki ijayo yaani Aprili 27, na mkuu wa Jamii ya Waislamu wa Ufaransa,
Nabil an Nasri, na mkuu wa jamii ya kupambana na chuki dhidi ya Uislamu,
Sami Dabbah, watahutubia waandamanaji na kusisitiza juu ya haki ya
Waislamu wa mji huo ya kuwa na msikiti. Jumuiya ya Kudumisha Udugu ya
mji wa Montrouge ndiyo iliyoitisha maandamano hayo na imewataka wananchi
wote wa Ufaransa kushiriki kwenye maandamano hayo. Ujenzi wa msikiti
katika mji wa Montrouge huko Ufaransa ulianza miaka minne iliyopita
lakini miezi miwili tu tangu kuanza ujenzi huo, manispaa ya mji huo
iliingilia kati na kuzuia kuendelea kujengwa sehemu hiyo ya ibada kwa
Waislamu. Waislamu wa Ufaransa walipigania sana haki yao hiyo na mwaka
huu wa 2013 wamepewa tena kibali ya kuendelea kujenga msikiti huo lakini
hivi sasa pia manispaa ya mji wa Montrouge imeingilia tena kati na
kuzuia ujenzi huo kwa madai kuwa Waislamu mjini humo ni wachache hivyo
hawana haki ya kuwa na msikiti.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment