Rais wa zamani wa Zambia Rupiah Banda ana haki ya kwenda mahakamani
kulalamikia kuondolewa kinga yake ya kutoshtakiwa. Jaji wa Mahakama Kuu
ya Zambia amesema kuwa, Banda ana haki ya kulalamikia maamuzi
yaliyotolewa na bunge la nchi hiyo ya kumuondolea kinga ya
kutoshitakiwa. Mnamo tarehe 15 Machi mwaka huu, bunge la Zambia
lilimuondolea kinga ya kutoshtakiwa Rupiah Banda ili apelekwe mahakamani
kujibu tuhuma zinazomkabili za kufanya ubadhirifu katika kipindi cha
miaka mitatu aliyokuwa madarakani. Rais wa zamani wa Zambia anakabiliwa
na tuhuma hizo amma wafuasi wake wanaamini kwamba, Rais Michael Sata wa
Zambia ndiye aliyepanga njama hizo kwa lengo la kumdhoofisha kisiasa
Rupiah Banda.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment