Wanajeshi watano wa Mali wameuawa baada ya helkopta ya kijeshi
waliyopanda kuanguka nchini humo. Jeshi la Mali limethibitisha kuanguka
kwa helkopta hiyo na wanajeshi wote watano waliokuwemo ndani ya chombo
hicho kupoteza maisha. Taarifa ya Jeshi la Mali imeeleza kuwa, helkopta
hiyo ilianguka jana katika eneo la Sevare kutokana na matatizo ya
kiufundi. Hata hivyo jeshi la Mali limeeleza kuwa, litafanya uchunguzi
zaidi ili kubaini chanzo cha ajali hiyo. Jeshi la Mali limetangaza
kuanguka kwa helkopta hiyo, huku kukiwa na uvumi kwamba wanamgambo waasi
ndio waliofanya shambulio la kuitungua helikopta hiyo.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment