Rais Hassan Sheikh Mahmoud wa Somalia
Mfuko wa Kimataifa wa Fedha IMF umeitambua rasmi serikali ya Somalia,
na kufungua pazia la kuboreshwa uhusiano wa pande mbili, baada ya IMF
kusitisha uhusiano wake na nchi hiyo yapata miaka 22 iliyopita. Taarifa
ya IMF imeeleza kuwa, hatua hiyo imechukuliwa kutokana na uungaji mkono
wa Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika, Umoja wa Ulaya na taasisi
nyingine za kimataifa kwa serikali inayoongozwa na Rais Hassan Sheikh
Mahmoud wa Somalia. Taarifa hiyo imeeleza kuwa, hivi sasa nchi hiyo ina
madeni ya dola milioni 352 hivyo haina sifa ya kupokea misaada mipya ya
kifedha kutoka mfuko huo. Tokea mwaka 1991, baada ya kuangushwa utawala
wa Muhammad Siad Barre, Somalia ilikuwa haina serikali kuu na hali hiyo
ilisababisha nchi hiyo kukumbwa na machafuko. Serikali ya Rais Hassan
Sheikh Mahmoud iliingia madarakani mwezi Septemba mwaka 2012 na mwezi
uliopita, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilisimamisha kwa muda
wa mwaka mmoja vikwazo vya silaha vilivyowekwa dhidi ya nchi hiyo
0 comments:
Post a Comment