Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Burundi zimetiliana saini mikataba minane kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa nchi hizi mbili.
Mikataba hiyo imetiwa saini hapa Tehran
katika kikao kilichohudhuriwa na Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Iran na
mwenzake wa Burundi Pierre Nkurunziza.
Mikataba iliyotiwa saini inahusu
ushirikiano katika uga wa kilimo, huduma ya utibabu wa mifugo, mafunzo
ya kiufundi, afya, masomo ya tiba, biashara na kuondolewa viza.
Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi
aliwasili Tehran siku ya Jumanne akiongoza ujumbe wa ngazi za juu kwa
lengo la kuimarisha uhusiano baina ya Iran na Burundi. Katika safari
yake hapa nchini Rais wa Burundi pia alikutana na kufanya mazungumzo na
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu mbali na kutembelea miradi
kadhaa ya maendeleo.
Hatua za kuimarisha ushirikiano wa Iran
na Burundi zinachukuliwa katika fremu ya siasa maalumu za Jamhuri ya
Kiislamu za kuzipa kipaumbele maalumu nchi za Kiafrika pamoja na azma
yake ya kuzidisha uhusiano na nchi hizo
0 comments:
Post a Comment