Nchini Kenya mvua za masika
zilizoanza mapema mwezi huu zimesababisha mafuriko makubwa. Watu 34
wamepoteza maisha na wengine elfu 26 wamebaki bila makao.
Shirika la Msalaba Mwekundu nchini Kenya
limetoa taarifa na kusema vifo vimeripotiwa katika maeneo ya Nyakach na
Homa Bay, Bura katika Mto Tana na eneo la Bondo la Ufa.
Peter Outa Afisa wa habari wa Shirika la
Msalaba Mwekundu nchini Kenya amesema idadi hiyo inahusu yale tu maeneo
ambayo waokoaji wa msalaba mwekundu wamefanikiwa kufika.
Idara ya Hali ya Hewa ya Kenya imesema
mvua kali zitaendelea kunyesha katika kipindi cha wiki mbili zijazo na
Wakenya wametakiwa kuchukua tahadhari. Mvua zinazonyesha Kenya
zimesababisha hasara kubwa kwa miundo mbinu hasa barabara na madaraja.
Wakati huo huo makamu wa rais wa Kenya
William Ruto jana usiku aliitisha kikao cha dharura na maafisa husika
kujadili mafurukio ambayo yamekumba maeneo kadhaa ya nchi hiyo. Ruto
amesema serikali itachukua hatua za dharura kutuma misaada ya
kibinaadamu kwa waathirika na kuongeza kuwa kuna mpango wa kutafuta
suluhisho la muda mrefu ili kuhakikisha mvua hazisababishi hasara kama
inavyoshuhudiwa kila mwaka.
0 comments:
Post a Comment