Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo amekutana na
kufanya mazungumzo na Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi mjini Tehran
ambapo Ahmadineajd amesisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiano wa nchi
hizi mbili.
Rais Ahmadinejad amesema mataifa ya Iran na Burundi yana
maadui wa pamoja na hivyo yanapaswa kushirikiana katika kukabiliana na
maadui.
Amesema nchi hizi mbili zitashirikiana katika mkondo wa ustawi
wa maendeleo na kuondoa umasikini. Rais Ahmadinejad amesema katika uga
wa kimataifa, Burundi imekuwa ikitetea haki za kimsingi za Jamhuri ya
Kiislamu ya Iran na hivyo Iran nayo iko pamoja na watu na serikali ya
Burundi katika juhudi zao za ustawi na maendeleo. Kwa upande wake Rais
Pierre Nkurunziza wa Burundi amesema uhusiano wa Tehran na Bujumbura ni
mpana na wenye mikakati. Amesema Burundi daima itakuwa pembeni mwa
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Rais Nkurunziza amesema mashirika ya Iran
yanakaribishwa kuwekeza katika sekta mbali mbali za Burundi. Rais Pierre
Nkunruziza wa Burundi, amewasili hapa mjini Tehran leo Jumanne kwa
ziara rasmi yenye lengo la kukutana na kufanya viongozi wa Jamhuri ya
Kiislamu ya Iran. Katika safari hii nchi mbili zitatiliana saini
mikataba kadhaa ya ushirikiano.
0 comments:
Post a Comment