Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Tuesday 30 April 2013

17 wauwa katika mapigano kaskazini mwa Nigeria




Kwa akali watu 17 wameuawa katika mapigano makali yaliyojiri kati ya askari jeshi wa serikali ya Nigeria na makundi yanayobeba silaha katika eneo la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Luteni Kanali A.G Laka amethibitisha kutokea mapigano hayo katika eneo la Bama, lililoko katika jimbo la Borno. Luteni Kanali Laka amesema kuwa, kwenye mapigano hayo maafisa saba wa polisi na askari wengine kumi waliuawa.
Hakuna kundi lolote lililotangaza kuhusina na shambulio hilo, lakini inashukiwa kwamba kundi la Boko Haram ndilo lililotekeleza shambulio hilo. Kundi la Boko Haram limekuwa likitekeleza operesheni  dhidi ya majengo ya serikali kama mashule, mahospitali na miundombinu mbalimbali katika eneo la kaskazini mwa Nigeria tangu mwaka 2009.

0 comments:

Post a Comment