skip to main |
skip to sidebar
MAONI YANGU KUHUSU KUULIWA KWA ASKARI POLISI-ZANZIBAR.
Uislam haujahalalisha damu ya MUUMINI kumwagwa na wala muumini
hajahalalishiwa kuimwaga damu ya muumini mwenzake.Na inapotokea mtu
akamwaga damu ya mwenzake na ni katika nchi yenye kutekeleza sheria ya
kiislam,basi mtu huyo lazima na yeye auwawe ili kuondoa chuki na fitna
kwa wale waliouliwa mtu wao.
Kwa jambo lililofanyika la kumuuwa huyo askari naweza kusema hili si la
halali na si katika matendo ya watu wenye imani ya kweli,lakini kwa
upande mwengine tujiulize,,kwanini askari huyu tu ndie alieuwawa, tena
kwa ghafla?????Akili yangu inaniambia kuwa,,kuuliwa kwa huyu askari
kunahitaji uchunguzi wa hali ya juu,maana watu wenye akili zao na imani
zao,hawawezi tu kutoka walikotoka wakaenda moja kwa moja kumuuwa huyu
askari,inawezekana na yeye alikuwa katika harakati fulani
fulani........................
Tuchukulie mfano mmoja tu,2001 kisiwani PEMBA, mambo waliyofanyiwa
wazee wetu na mama zetu na hao hao askari, mengine hata hayasemeki,na
WALLAH wengine walikuwa ni WAZANZIBAR wenzetu( MKUU WA KITUO CHA POLISI
CHA KASKAZINI PEMBA.), na kwa bahati nzuri sisi nyumbani waliweza hata
kuingia mpaka ndani(BAADA YA KUVUNJA MLANGO),tukawa na uwezo wa
kuwasikia lafdhi zao,kwa kweli ni waznz wenzetu,watu wa bara walikuwa
wachache,japo walikuwepo.
Sasa haya yote yalitendeka lakini tokea
kipindi hicho sijawahi kusikia askari kachinjwa na kuuliwa,na hao askari
wapo mpaka leo.SASA KWANINI AWE NI ASKARI HUYU TU tena katika jimbo la
bububu ambalo hivi karibuni tu yalitokea machafuko ambayo yalipelekea
majeraha makubwa kwa watu?
Mimi nafikiri kuna kundi maalum ambalo hujiingiza katika vurugu kama
hizi ilimradi tu kile kinachopiganiwa kisipatikane.Nanukuu kauli ya shkh
MSELLEM aliposema"KATIKA MSAFARA WA MAMBA,NA KENGE WAMO" .Na
inawezekana wao ndio waliosababisha kifo cha askari huyu.(MUNGU AMSAMEHE
MAKOSA YAKE).
Kwa hivyo ndugu zangu nawashauri,sio kila baya
linalotendeka katika harakati zilizopo sasa,tusikurupuke tu na kusema
kwamba waliofanya hivyo ni UAMSHO ama ni WAISLAM.Siwezi kuamini kuwa
wanaovunja BAA na MADUKA ya watu wakaiba kila kitu na kufikia hatua ya
kunywa POMBE,wote hawa ni uamsho au ni waislam!!!!!
LAZIMA TUFIKIRIE MARA MBILIMBILI KABLA YA KUTOA MAAMUZI KATIKA AKILI ZETU.muumini wa kweli,mambo kama haya hawezi kufanya.
NAPENDA KUWAPA POLE WALE WALIOFIKWA NA MSIBA HUU,NA NAPENDA KUISHAURI
SERIKALI YA ZANZIBAR,KAMA KWELI WAO HAWAHUSIKI NA JAMBO HILI LA KUTEKWA
NYARA KIONGOZI WA UAMSHO,BASI NI VYEMA KUCHUKUWA HATUA ZA HARAKA KATIKA
KUPATIKANA KWAKE ILI KUONDOA FIKRA MBAYA KWA WANANCHI WAO.
SERIKALI
INATAKIWA IELEWE KUWA,HUYU NAE NI RAIA NA ANA KILA HAKI YA KULINDWA KAMA
ANAVYOLINDWA RAIS.NA WAELEWE KUWA BAYA LOLOTE LITAKALOTOKEA KWAKE(KAMA
NI KIFO AU KUTOKUONEKANA TENA,MUNGU AMUHIFADHI) BASI NCHI HAITOKUWA NA
AMANI TENA NA WALA WANANCHI HAWATOKUWA NA IMANI TENA NA VIONGOZI
WAO(Allah anusuru tusifike huko)
Hivi tujaalie kama alietekwa
ni KATIBU MKUU WA CCM-ZANZIBAR,hali ya viongozi wetu
ingekuwaje?wangelinyamaza na kusema kuwa,wanafuatilia?Mi nafikiri
wangelikwishachukuwa hatua za haraka,hata kukodi majeshi kutoka nje ya
ZNZ ili apatikane,sasa wawili hawa wana tofauti gani katika sheria na
ulinzi?
Natumai viongozi wetu ni waelewa na wasikivu.
WABILLAH ATAWFIQ.
0 comments:
Post a Comment