Na Veronica Kazimoto – MAELEZO
Dar es Salaam
18.10.2012
.
Sikukuu ya Eid-El-Hajj itakuwa siku ya tarehe 26 Ockoba mwaka huu ambapo
kitaifa swala itafanyika katika msikiti wa Vuchama wilayani Mwanga katika mkoa
wa Kilimanjaro ikifuatiwa na Baraza la Eid baada ya Swala.
Kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi wa habari na mawasiliano ya Umma Simba
Shabani wa Baraza Kuu la Waislam wa Tanzania (BAKWATA) mgeni rasmi
anatarajiwa kuwa kuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya
Kikwete.
Taarifa hiyo imefafanua kuwa sababu ya tarehe hiyo ni kutokana na siku hii ya leo
kuwa mwezi tatu, Dhul-Hijja mwaka 1433 kwa mujibu wa kalenda ya Kiislam.
Aidha Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Issa Bin Shaaban Simba amewataka
Waislam wote nchini kusherehekea kwa amani na utulivu sikukuu hiyo huku
wakichunga mipaka ya Allah (S.W).
Sheikh Shaaban Simba pia amewataka waislamu kutii sheria za nchi na kuepukana
na watu ambao wanataka keleta tafrani za kidini hapa nchini.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment