Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 4 July 2013

Kenya yakanusha kuunga mkono machafuko Kismayo

                              

Wizara ya Ulinzi ya Kenya imekanusha tuhuma kwamba jeshi la nchi hiyo linachochea machafuko katika mji wa Kismayo, Kusini mwa Somalia. Taarifa ya wizara hiyo imesema jeshi la Kenya linafanya juu chini kuona amani na utulivu vinarejea Somalia. Serikali ya Somalia imelituhumu jeshi la Kenya kwamba limeshindwa kufanya kazi barabara na hivyo kusababisha mapigano ya hivi karibuni kati ya makundi tofauti yaliyosababisha vifo vya watu 65. Serikali ya Mogadishu imeuandikia barua Umoja wa Afrika ikisema Kenya imekuwa ikiegemea upande mmoja na kulipendelea kundi moja dhidi ya makundi mengine na ilimkamata afisa mmoja mkuu wa jeshi la Somalia akitumia silaha nzito katika maeneo ya raia katika eneo la Kismayo, kusini mwa Somalia. Kenya ina kikosi chake kusini mwa Somalia karibu na mpaka wake kama sehemu ya kikosi cha Umoja wa Afrika cha kulinda amani. Somalia imekuwa katika vita kwa miongo kadhaa sasa lakini matumaini yalikuwa kwamba kikosi cha Umoja wa Afrika wakiwemo wanajeshi wa Kenya wataleta tofauti kubwa katika nchi hiyo. Sasa Somalia inautaka Umoja wa Afrika kuchunguza madai hayo na iwapo yatabainika kuwa ya kweli basi jeshi la Kenya liondolewe nchini humo.
 

0 comments:

Post a Comment