Mkutano wa 11 wa Bunge la Muungano unaendelea leo baada ya
mapumziko ya mwishoni mwa wiki, huku wabunge na wananchi wakisubiri
Bajeti ya Serikali.
Baada ya wizara 32 kumaliza kuwasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2013/14, kinachosubiriwa sasa ni bajeti kuu.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, wabunge walikamilisha
michakato ya kupitisha maombi ya fedha kila wizara, tayari wizara zote
zinasubiri kasma ya Serikali kwa shughuli za kawaida na maendeleo.
Wakati hayo yakiendelea, Kamati ya Bajeti nayo
ilikuwa hatua za mwisho kukamilisha kazi yake ya kutengeneza mazingira
ya mwelekeo wa bajeti hiyo kabla ya Bajeti Kuu itakayowasilishwa siku
nne zijazo.
Katika kuweka sawa hilo, wizara licha ya
kuwasilisha makadirio ya mapato na matumizi bungeni kwa mwaka 2013/14,
ziliwasilisha kwenye kamati hiyo ili kuona jinsi ya kusaidia na
kurahisisha utekelezaji bajeti husika kila wizara na idara zake.
Changamoto kubwa katika utekelezaji bajeti kwa
mwaka 2013/14, ni upatikanaji fedha ambazo licha ya kutoka Serikali Kuu,
zinategemea fedha za wahisani ili kukamilisha bajeti hiyo.
Katika mkutano huu ambao unaendelea mjini hapa,
Bunge lilianza na makadirio ya mapato na matumizi ya wizara zilizo chini
ya Ofisi ya Waziri Mkuu na kuhitimisha na Wizara ya Fedha.
Shughuli nyingine ambayo imekwisha kufanyika hadi
sasa, ni uchaguzi wa wajumbe katika uwakilishi wa taasisi mbalimbali,
vyuo vikuu na Jumuiya ya Uchumi Kudini mwa Afrikaa (SADC).
Kwa utaratibu wa kawaida, Alhamisi asubuhi, Bunge
litaanza kwa kupokea taarifa ya hali ya uchumi ambayo itasomwa na waziri
mwenye dhamana ya Mipango ya Uchumi kabla ya jioni kusomwa Bajeti Kuu.
Ratiba ya Bunge inaonyesha baada ya kusomwa kwa
Bajeti Kuu, siku hiyo mchana Bunge litaahirishwa ili kuwapa nafasi
wabunge kuipitia kabla ya Jumatatu wiki ijayo kuanza kujadiliwa kwa siku
saba.
0 comments:
Post a Comment