Uvaaji wa
hijabu na nguo nyingine zenye kuonyesha nembo ya kidini umepigwa marufuku
kwenye mashule na vyuo vikuu vya kusini mwa Russia.
Gavana wa Jimbo la
Astrakhan nchini Russia amesema kuwa, kuanzia mwezi Septemba mwaka huu ni
marufuku kuvaa mavazi yenye kuonyesha nembo ya kidini kwenye shule na vyuo
vikuu vilivyoko katika jimbo hilo.
Ameongeza kuwa, Russia ni nchi ya kisekula,
hivyo inapasa kukabiliana na baadhi ya makundi ya kikabila na kidini yanayotaka
kudhihirisha itikadi na imani zao kwenye taasisi za elimu katika eneo
hilo.
Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka 2012, asilimia 46 ya wananchi wa
jimbo la Astrakhan ni Wakristo wa Madhehebu ya Orthodox, asilimia 16 ni
Waislamu na iliyosalia ni wafuasi wa dini na madhehebu nyinginezo.
0 comments:
Post a Comment