Mahakama ya Cairo Jana imewahukumu bila kuwepo mahakamani, raia wa kigeni
wapatao 27 wakiwamo Wamarekani 16 kwa tuhuma za kutoa misaada ya
kifedha kwa taasisi tofauti za nchi hiyo, kinyume cha sheria. Ripoti
zinasema kuwa, watuhumiwa hao wamehukumiwa kifungo cha miaka mitano
jela. Kabla ya hapo serikali ya Cairo, ilikuwa imetangaza kuwahukumu
raia wa kigeni 44 wakiwamo Wamarekani 19, kwa tuhuma za kuzisaidia
taasisi binafsi za nchi hiyo, kinyume cha sheria. Kwa mujibu wa serikali
ya Misri, watuhumiwa hao ni raia wa Ujerumani, Marekani, Norway,
Serbia, Jordan na Palestina. Habari zinasema kuwa, raia hao wa kigeni
waliingi kinyemela nchini humo, wakati wa kujiri mapinduzi ya wananchi
dhidi ya utawala wa dikteta Hosni Mubarak, kwa lengo la kuzusha fitina
nchini.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment