Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Tuesday 4 June 2013

Maandamano mbele ya ofisi ya Waziri Mkuu wa Uturuki

                             
 Huku maandamano makubwa yakiwa bado yanaendelea dhidi ya serikali ya Uturuki, mamia ya waandamanaji leo wamefanya maandamano mbele ya ofisi ya Waziri Mkuu wa nchi hiyo Receb Tayyip Erdogan. Waandamanaji hao waliokuwa wamejawa na hasira, wamekabiliana vikali na polisi katika eneo hilo. Machafuko hayo yaliyoanza siku ya Alkhamisi iliyopita mjini Istanbul na kuenea karibu maeneo yote ya Uturuki, yamesababisha watu kadhaa kuuawa huku zaidi ya wangine 200 wakijeruhiwa na maelfu kutiwa mbaroni. Hii ni katika hali ambayo, jumuiya ya wafanyakazi nchini humo, imetangaza mgomo wa siku mbili wa wafanyakazi kuanzia leo, kulalamikia ukandamizaji wa kufurutu mipaka unaofanywa na serikali dhidi ya waandamanaji. Wakati huo huo ofisi za ndege nchini Uingereza na Italia, zimetangaza kupunguza asilimia 30 ya safari za kitalii nchini Uturuki. Sekta ya utalii huiingizia nchi hiyo fedha nyingi za kigeni, ambapo kwa mwaka serikali ya Ankara hupata kiasi cha dola bilioni 22. Maandamano ya kupinga serikali ya nchi hiyo yameendelea katika miji ya Istanbul, Ankara, Izmir, Mugla na Antalya.

0 comments:

Post a Comment