Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Sunday 2 June 2013

Membe: Tanzania haiwezi kuiomba radhi Rwanda

                                    24Rajab,1434 Hijiriyah/ JUNY 03,2013 Miyladiyah
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania, Bernard Membe amesema kuwa, kamwe Tanzania haitaiomba radhi Rwanda, baada ya Rais Jakaya Kikwete kuishauri nchi hiyo kufanya mazungumzo na upinzani ili kumaliza vita katika eneo la Maziwa Makuu. Serikali ya Rwanda ilikuwa imeitaka Tanzania iombe radhi kwa madai kuwa kauli ya Rais Kikwete ni kama tusi kwao na kwamba wao hawawezi kukaa na kuzungumza na wapinzani ambao ni wauaji. Membe amesema kama ninavyomnukuu: “Kama Rwanda haitaki kufuata ushauri wa Rais Kikwete inatakiwa kuuacha na siyo kumtaka aombe radhi,” mwisho wa kunukuu. Membe aliyasema hayo jana alipokuwa akitoa ufafanuzi huo bungeni. Tamko hilo la Serikali ya Tanzania limekuja ikiwa zimepita takriban siku sita tangu serikali ya Rwanda itowe tamko la kupinga ushauri huo uliotolewa na Rais Kikwete wakati akiwa katika sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU), uliofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia.

0 comments:

Post a Comment