Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Tuesday 18 June 2013

Generali David Sejusa avunja kimya chake

                            
Jenerali wa Jeshi aliyesababisha hali ya mshikemshike au sekeseke nchini Uganda wakati maudhui ya barua aliyoiandika yalipofichuka hadharani amezungumza na BBC kwa mara ya kwanza.

Generali David Sejusa, mmoja wa maafisa wa juu katika jeshi la Uganda alitaka kufanyike uchunguzi wa tuhuma kuwa kuna mpango wa kuwaua maafisa waandamizi wa jeshi na wa serikali wanaopinga kile kilichotajwa kuwa ni mradi wa Muhoozi, mtoto wa Rais Museveni akiandaliwa
Magazeti mawili na vituo vya Radio vilifungwa kwa karibu siku kumi wakati maafisa usalama walipokuwa wakijaribu kutafuta barua hiyo.

Tangu barua hiyo ilipotolewa hadharani, Jenerali huyo amekuwa kama yuko mafichoni.
Sejusa anasema kuwa yeye ndiye aliyendaika barua hiyo ila hafahamu vipi ilifika mikononi m,wa vyombo vya habari.

Aidha Sejusa amelaani hatua ya serikali kushambulia vyombo vya habari baada ya barua hiyo kufichuliwa akisema kuwa yeye ndiye alikuwa mwandishi wa barua yenyewe na kuwa serikali ingemsubiri arejee Uganda ndiposa iweze kumhoji kuhusu maudhui ya barua hiyo.

Akizungumza na BBC Swahili, Jenerali Sejusa alisema tatizo kubwa na kitu ambacho anakipagia Uganda ni kutaka kuweka muda ambao rais anapaswa kutawala nchio hiyo. Amelaani uongozi wa Rais Yoweri Museveni akisema kuwa katiba ya nchi inapaswa kulindwa kwa njia yoyote labda hata kutumia nguvu dhidi ya wale wanaoikiuka.

Hata hivyo Serikali ya Uganda imepuuzilia mbali madai hayo ya Jenerali David Sejusa. Akizungumza na BBC, msemaji wa serikali ya Uganda Ofwono Opondo, amesema madai hayo hayana msingi wowote.

Aidha amesema Uganda inatawaliwa kwa misingi ya katiba ya nchi hiyo na ikiwa Jenerali huyo ana malalamiko ya kikazi au kiutawala anaweza kutumia njia ambazo zimewekwa na katiba ya Uganda.


 

0 comments:

Post a Comment