Jenerali wa Jeshi aliyesababisha
hali ya mshikemshike au sekeseke nchini Uganda wakati maudhui ya barua
aliyoiandika yalipofichuka hadharani amezungumza na BBC kwa mara ya kwanza.
Generali David Sejusa, mmoja wa
maafisa wa juu katika jeshi la Uganda alitaka kufanyike uchunguzi wa tuhuma
kuwa kuna mpango wa kuwaua maafisa waandamizi wa jeshi na wa serikali
wanaopinga kile kilichotajwa kuwa ni mradi wa Muhoozi, mtoto wa Rais Museveni
akiandaliwa
Magazeti mawili na vituo vya Radio
vilifungwa kwa karibu siku kumi wakati maafisa usalama walipokuwa wakijaribu
kutafuta barua hiyo.
Tangu barua hiyo ilipotolewa
hadharani, Jenerali huyo amekuwa kama yuko mafichoni.
Sejusa anasema kuwa yeye ndiye
aliyendaika barua hiyo ila hafahamu vipi ilifika mikononi m,wa vyombo vya
habari.
Aidha Sejusa amelaani hatua ya
serikali kushambulia vyombo vya habari baada ya barua hiyo kufichuliwa akisema
kuwa yeye ndiye alikuwa mwandishi wa barua yenyewe na kuwa serikali ingemsubiri
arejee Uganda ndiposa iweze kumhoji kuhusu maudhui ya barua hiyo.
Akizungumza na BBC Swahili, Jenerali
Sejusa alisema tatizo kubwa na kitu ambacho anakipagia Uganda ni kutaka kuweka
muda ambao rais anapaswa kutawala nchio hiyo. Amelaani uongozi wa Rais Yoweri
Museveni akisema kuwa katiba ya nchi inapaswa kulindwa kwa njia yoyote labda
hata kutumia nguvu dhidi ya wale wanaoikiuka.
Hata hivyo Serikali ya Uganda
imepuuzilia mbali madai hayo ya Jenerali David Sejusa. Akizungumza na BBC,
msemaji wa serikali ya Uganda Ofwono Opondo, amesema madai hayo hayana msingi
wowote.
Aidha amesema Uganda inatawaliwa kwa
misingi ya katiba ya nchi hiyo na ikiwa Jenerali huyo ana malalamiko ya kikazi
au kiutawala anaweza kutumia njia ambazo zimewekwa na katiba ya Uganda.
0 comments:
Post a Comment