Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Sunday 30 June 2013

Ethiopia yapendekeza mazungumzo ya kweli na Misri

                                22 shaaban,1434 Hijiriyah/ 01 july,2013 Miyladiyah


Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia ametaka yafanyike mazungumzo kati ya nchi yake na Misri juu ya tofauti za ujenzi wa bwawa la Renaissance. Tedros Adhanom Ghebreyesus ameyasema hayo katika kikao cha pamoja na waandishi wa habari kati yake na Murad Mudallis waziri mwenzake wa Mambo ya Nje wa Algeria na kuongeza kuwa, nchi yake inataka kumaliza baadhi ya tofauti zilizosalia kuhusiana na kadhia hiyo. Aidha Ghebreyesus ameongeza kuwa, hivi karibuni atafanya safari nchini Misri kuitikia wito wa Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa nchi hiyo Mohamed Kamel Amr kuhusiana na kadhia hiyo. Hatua ya Ethiopia ya kutaka kujenga bwawa la Renaissance katika mto Nile, ilikabiliwa na radiamali kali ya srikali ya Cairo na kuibua suutafahumu kati ya nchi mbili hizo. Misri inaitaka serikali ya Addis Ababa kufungamana na mkataba wa zamani kuhusiana na utumiaji wa maji ya mto huo, mkataba ambao unaipa zaidi Misri na Sudan haki ya kustafidi na maji ya mto huo,  suala linalopingwa na Ethiopia inayosisitiza juu ya mkataba wa Entebbe, Uganda unaozipa haki sawa nchi zote zinazochangia maji ya mto huo.

0 comments:

Post a Comment