Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday 15 June 2013

Ban na Mursi: Mgogoro wa Syria utatuliwe kisiasa

                            
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki moon na Rais Muhammad Mursi wa Misri, wamesisitizia haja ya kutatuliwa mgogoro wa Syria kwa njia za kisiasa. Habari zinasema kuwa, viongozi hao wamefikia makubaliano hayo kupitia njia ya simu sambamba na Ban Ki moon kushukuru juhudi za kidiplomasia zinazofanywa na Cairo kuhusiana na kadhia ya Syria. Aidha mazungumzo hayo yalijalidi hali ya Syria na kuitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua za lazima za kukomesha umwagaji damu nchini humo na kuanza mchakato wa kisiasa wa kutatua mgogoro huo. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Rais Muhammad Mursi, amesisitizia udharura wa kuharakishwa mkutano wa Geneva 2 na kuongeza kuwa, Cairo itawasilisha mtazamo wake katika kikao hicho. Ban Ki moon na Rais Mursi wa Misri pia wamezungumzia ripoti ya Tume ya Pande Tatu inayofuatilia na kuchunguza athari za ujenzi wa bwawa la an-Nahdha la Ethiopia ambapo Rais Musri alisisitiza kuwa, Misri yenye uchumi mzuri zaidi kati ya nchi nchi zinazopakana na mto Nile, italinda maslahi ya nchi za jirani kwa sharti Cairo isiathiriwe na matumizi ya nchi nyingine ya maji ya mto huo.

0 comments:

Post a Comment