Mjumbe moja wa Kamati ya Utendaji ya Kituo cha Uchaguzi nchini
Iran amesema kuwa, hadi anatangaza habari hiyo, zaidi ya asilimia 70 ya
watu waliotimiza masharti ya kupiga kura mjini Tehran walikuwa tayari
wameshiriki katika duru ya 11 ya uchaguzi wa rais na duru ya nne ya
uchaguzi wa mabaraza ya miji na vijiji hapa nchini.
Bw. Ismail Kauthari ameongeza kuwa wanatabiri kuwa asilimia 70 ya wananchi wa Tehran wamejitokeza kupiga kura huku idadi kubwa zaidi ya watu waliopiga kura ikiwa ni ya wananchi wa mikoani na vijijini.
Hadi tunapokea habari hii, upigaji kura ulikuwa bado unaendelea na ulikuwa tayari umeshaongezewa muda kwa mara kadhaa jambo ambalo linaonesha wazi kuwa asilimia ya watu walioshiriki kwenye zoezi hili muhimu itakuwa zaidi ya hiyo.
Bw. Ismail Kauthari ameongeza kuwa wanatabiri kuwa asilimia 70 ya wananchi wa Tehran wamejitokeza kupiga kura huku idadi kubwa zaidi ya watu waliopiga kura ikiwa ni ya wananchi wa mikoani na vijijini.
Hadi tunapokea habari hii, upigaji kura ulikuwa bado unaendelea na ulikuwa tayari umeshaongezewa muda kwa mara kadhaa jambo ambalo linaonesha wazi kuwa asilimia ya watu walioshiriki kwenye zoezi hili muhimu itakuwa zaidi ya hiyo.
0 comments:
Post a Comment