Ibrahim Ibrahim, Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Afrika Kusini
Ibrahim
Ibrahim Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Afrika Kusini amesema kuwa,
nchi hiyo imeshaanza kupeleka wanajeshi wake katika eneo lililogubikwa na
machafuko la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo chini ya mwamvuli
wa vikosi maalumu wa Umoja wa Mataifa vya kupambana na waasi nchini humo. Naibu
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Afrika Kusini ameongeza kuwa, jumla ya
wanajeshi 1345 wa nchi hiyo watapelekwa nchini Kongo, chini ya mwamvuli wa
vikosi maalumu vya Umoja wa Mataifa. Nchi za Tanzania na Malawi zimeshapeleka
wanajeshi wake 3,000 katika mji wa Goma ulioko mashariki mwa Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo tokea mwezi Mei uliopita.
0 comments:
Post a Comment