Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday 27 June 2013

39 wauawa katika mapigano ya kikabila Sudan

 
Mapigano ya kikabila yaliyozuka kaskazini mwa jimbo la Darfur, Sudan, yamepelekea watu 61 kuuawa na wengine wengi kujeruhiwa. 
Mapigano hayo yalizuka jana yakiyahusisha makabila mawili ya Bani Hussein na Illa Balah katika eneo la al-Sarif kaskazini mwa jimbo hilo na kupelekea watu 39 kuuawa na wengine 22 kujeruhiwa. 
Katika mapigano hayo watu wengine kadhaa wametoweka.
 Kiongozi wa baraza lililoundwa hivi karibuni kwa minajili ya kukabiliana na migogoro ya eneo la mji huo ‘al-Sarif’ Bwana Ahmad Mahdi Hamid, ameitaka serikali ya Khartoum kufanya juhudi zaidi za kumaliza mapigano kati ya makabila hayo mawili na kusisitizia udharura wa kunyang’anywa silaha wanamgambo wa makabila hayo. Amesema silaha hizo zimekuwa sababu kubwa ya kuyaingiza makabila kadhaa nchini humo katika mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.
 Hivi karibuni Rais Omar Hasan al Bashir wa Sudan alionya juu ya hatari ya mapigano ya kikabila ambayo yamekuwa yakitokea katika baadhi ya maeneo ya nchi hiyo na kuyataja kuwa ni hatari kwa usalama wa taifa. Al Bashir alisema hayo katika kikao cha Baraza la Ushauri la Kongresi ya Taifa na kuongeza kuwa, serikali yake inakabiliwa na changamoto kubwa katika kuzuia hali hiyo. 
Wakati huo huo taarifa zinaeleza kuwa, serikali ya Sudan, imeanza tena kusafirisha mafuta ya Sudan Kusini kupitia mabomba na bandari zake za usafirishaji mafuta.

0 comments:

Post a Comment