03,RAJAB,1434 Hijiriyah/ May 13,2013 Miyladiyah
Serikali ya Mali imetangaza kuwa, imewapeleka askari wake karibu na mji
wa Kidal kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Habari zaidi zinasema kuwa,
hatua hiyo imefanyika kwa minajili ya kuusafisha mji huo kutokana na
wanamgambo waasi. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, serikali ya Mali inafanya
juhudi za kuudhibiti mji huo, kabla ya uchaguzi wa bunge na rais
uliopangwa kufanyika mwezi Julai mwaka huu. Siku ya Jumanne iliyopita,
muungano wa viongozi wa jumuiya ya Waislamu nchini Mali, ulikosoa vikali
hatua ya serikali kushindwa kutuma askari wake katika mji wa Kidal
unaodhibitiwa na wanamgambo wa Kituareg. Hii ni katika hali ambayo, hivi
karibuni kundi la Watuareg lilitangaza kuwa, litatoa jibu kali ikiwa
askari wa Mali watajaribu kuingia katika ameneo yanayodhibitiwa na kundi
hilo. Wakati huohuo Mawaziri wa ulinzi wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi
za Magharibi mwa Afrika ECOWAS walikutana nchini Ivory Coast na kujadili
hali ya mambo inayotawala nchini Mali, huku Waziri wa Mambo ya Nje wa
Mali Tieman Kolibaly akimtaka Rais Blaisse Compaore wa Burkinafaso
kufanya juhudi kubwa za kutuliza hali ya mambo katika mji wa Kidal ambao
ungali unashikiliwa na waasi wa Tuareg.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment