Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday 11 May 2013

DC CHUNYA AKEMEA MAUWAJI YANAYOTOKANA NA IMANI ZA KISHIRIKINA.............

                                02,RAJAB,1434 Hijiriyah/ May 12,2013 Miyladiyah

KUFUATIa mauaji ya kishirikina yaliyoibuka kwa kasi Mkoani Mbeya hivi karibuni ,MKUU wa Wilaya ya Chunya ,Bw. Deodatusi Kinawiro amewataka Madiwani wa halmashauri hiyo kukemea maovu hayo ambayo yameanza kuonyesha sura mbaya ya wilaya hiyo kwa watu wa nje.
 
Hatua hiyo inafuatiwa na mauaji hayo kushamili mwishoni mwa wiki katika kata ya Mwajuni mtaa wa Maweni kwa kikonge mmoja ambaye alikuwa mzee wa kanisa kuuwawa kwa imani za kishirikina kisha kufukiwa kaburi moja na marehemu baada ya kutuhumiwa kumroga kijana mmoja kijijini hapo.
 
Bw. Kinawiro aliyasema hayo jana wakati akizungumza na mtandao huu  kuhusiana na mauaji ya kishirikina yaliyoshamiri Wilayani humo na kuanza kuwatua hofu wananchi wanaotoka maeneo mbali mbali ya mikoa jirani kwa ajili ya kutafuta maisha.
 
“Kwa ujumla hivi sasa wilaya imekuwa na viashirio vya mauaji mengi sana yanayohusisha ushirikina wa ajabu , ulevi wa kupita kiasi ambao unasababisha vifo vingi sana katika wilaya mfano huyu mzee mstaafu wa kanisa aliyeuwawa hivi karibuni kwa visa tu na kuanza kumtuhumu uchawi kwa kuanza kumpiga mawe na kisha kumzika kaburi moja na marehemu “alisema Mkuu huyo wa Wilaya.
 
Hata hivyo Bw. Kinawiro aliwataka madiwani kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa wanatemvelea katika kata zao na kuongea na wananchi kuelimisha madhara ya kuamini ushirikina ambayo mpaka sasa yamekuwa kero kubwa na hqata kuwafanya wananchi waishi kwa hofu .
 
“Mi nashangaa sana kwanini wananchi wawe na imani potofu kiasi hiki kwanini isijulikane kuwa mtu ameumwa ugonjwa wa maralia lakini nashangaa sana kuona wananchi wakimbilia uchawi, hii haivumiliki hata kidogo vinginevyo hali hii ikiendelea kutakuja kutokea maafa makubwa”alisema Mkuu huyo.
 
Mkuu huyo wa Wilaya aliendelea na kuongeza kuwa madiwani walio wengi wapo karibu na wananchi kiasi kwamba wana uwezo mkubwa wa kuhakikisha hili linakwisha na kurudisha amani kwa wananchi na watu wengine wa nje.
 
Aidha Bw.Kinawiro aliwalaumu Makatibu tarafa kwa tabia zao za kukaa kimnya na taarifa za migogoro ambazo zimekuwa zikitokea na hivyo baadae kutokea vifo wakati uwezekano wa kulitafutia ufumbuzi ulikuwepo.
Mwisho.
"Chanzo Francis Godwin"

0 comments:

Post a Comment