Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Tuesday 2 April 2013

Watu 13 wafariki katika hujuma dhidi ya Waislamu Myanmar 21,Jumaadal ula,1434Hijiriyah/ Murch 02,2013Miyladiyah

                                 21,Jumaadal ula,1434Hijiriyah/ April 03,2013Miyladiyah
 Watu 13 wamefariki dunia kutokana na moto ulioteketeza shule ya Waislamu nchini Myanmar. Moto huo uliotokea leo katika mji wa Yangon nchini humo, umezusha hasira kali kwa wakazi wa eneo hilo kutokana na serikali kushindwa kudhibiti vitendo vya kikatili vinavyotekelezwa dhidi ya Waislamu, licha ya ahadi ambazo zimekuwa zikitolewa na watawala wa nchi hiyo za kukabiliana na wahalifu. Aidha habari zaidi zinasema kuwa, wakati moto huo ukitokea katika shule hiyo iliyokaribu na msikiti, zaidi ya watu 70 walikuwa wamelala. Polisi imetangaza kuanzisha uchunguzi katika tukio hilo huku ikidai kuwa, huenda moto huo ulisababishwa na hitilafu ya umeme. Kutokana na kuongezeka vitendo vya jinai dhidi ya Waislamu wa Myanmar, Jamii ya Waislamu wa nchi hiyo inaishi katika hali ya wasiwasi na hofu kubwa. Hii ni katika hali ambayo, jumuiya za kimataifa zimeendelea kufumbia macho jinai hizo. Kufuatia hali hiyo, Sheikh Abdul Alim Mussa imam wa msikiti wa al-Islam wa mjini Washington, Marekani hivi karibuni alinukuliwa akisema kuwa, nchini Myanmar kunaendelea vita vya dunia dhidi ya Waislamu huku Umoja wa Mataifa ukiwa umenyamaza kimya.

0 comments:

Post a Comment