22,Jumaadal ula,1434Hijiriyah/ April 03,2013Miyladiyah
Korea Kaskazini imetangaza kuwa itazindua upya kituo chake kikuu cha
nyuklia katika eneo la Yongbyon huku ngoma za vita zikiendelea kupigwa
katika Peninsula ya Korea.
Shirika rasmi la habari la nchi hiyo KCNA limesema kituo cha
kurutubisha madini ya urani na tanuri nyuklia tano ambazo zilifungwa
mwaka 2007 kama sehemu ya mkataba wa kuangamiza silaha, zitaanza kufanya
kazi upya katika Taasisi ya Nyuklia ya Yongbyon.
Msemaji wa miradi ya nishati ya nyuklia ya Korea Kaskazini amesema
hatua hiyo ni katika fremu ya sera za kujiimarisha kwa zana za nyuklia
na vile vile kutatua matatizo sugu ya ukosefu wa umeme. Jumatatu Korea
Kaskazini ilitangaza kuwa sera zake kuu kitaifa ni kuwa na uchumi wenye
nguvu na kuzalisha silaha za nyuklia. Siku hiyo hiyo Marekani ilitangaza
kutuma meli zake za kivita katika Peninsula ya Korea kwa lengo la
kukabiliana na makombora ya Korea Kaskazini. Aidha ndege za kivita za
Marekani aina ya F-22 zenye uwezo wa kukwepa rada zimefanya mazoezi
katika eneo hilo. Katika upande mwingine Rais wa Korea Kusini, Park
Geun-hye amesema nchi yake itajibu haraka hujuma kutoka nchi jirani ya
Korea Kaskazini. Korea Kusini na Korea Kaskazini ziliwahi kupigana vita
vikali kati ya mwaka 1950 – 1953 na kisha kusaini makubaliano ya
usitishaji vita kufuatia mashinikizo ya Umoja wa Mataifa,
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment