Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Tuesday 23 April 2013

Waliofukiwa mgodini waokolewa wakiwa hai

                 

 

 Watu wanne wamenusurika kufariki dunia baada ya udongo wenye mawe kuwafukia chini katika shimo zaidi ya saa 12 walipokuwa wakichimba dhahabu katika Kijiji cha Patamela wilayani Chunya.
Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Deodatus Kinawiro alithibitisha k wa njia ya simu jana juu ya tukio hilo na kwamba lilitokea Ijumaa iliyopita, ambapo uokoaji ulifanywa na Kampuni ya Shanta Gold Mining inayochimba dhahabu kilometa 10 kutoka eneo la tukio.
Kinawiro aliwataja walionusurika kuwa ni Antony Rwegasira(28), Pascal Claud(33) , John Gideon(47) na Noni Kwandu (40) wote wakazi wa wilayani humo.
CHANZO MWANANCHI.

0 comments:

Post a Comment