Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday 20 April 2013

US yatakiwa iache poropaganda chafu dhidi ya Sudan

                                        11Jumaadal Aakhir,1434 Hijiriyah/ April 21,2013 Miyladiyah 

Serikali ya Sudan imeionya Marekani na propaganda zake chafu za kisiasa dhidi ya Khartoum na kusisitiza kwamba, hatua ya Washington ya kuwataka Wamarekani wajihadhari na kufanya safari nchini Sudan ni ya kisiasa. Taarifa ya Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Sudan imesisitiza kwamba, tangazo hilo la Marekani lina malengo na matashi ya kisiasa. Abubakar Siddiqi, Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Sudan amesema kuwa, tahadhari hiyo ya Marekani sio jambo jipya.
Jana Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani iliwataka raia wake wajihadhari kufanya safari nchini Sudan hususan katika maeneo yanayokabiliwa na machafuko ya jimbo la Darfur, Kordofan Kusini na Blue Nile. Hata hivyo viongozi wa Khartoum wameitathmini tahadhari hiyo kwamba, ni muendelezo wa siasa chafu za Marekani dhidi ya Sudan. Hivi karibuni viongozi wa Sudan walisisitiza kwamba, viongozi wa Magharibi hususan wa Marekani wamekuwa wakifanya njama za kuonyesha kwamba, nchini Sudan hakuna amani ili kwa njia hiyo waweze kunufaika kisiasa na jambo hilo.

0 comments:

Post a Comment