11Jumaadal Aakhir,1434 Hijiriyah/ April 21,2013 Miyladiyah
Bango linalowaonyesha watu wakipashana uvumi na maandishi yanayo toa wito kwa Wanigeria 'kusema la kwa waeneza uvumi'
Wakuu wa jimbo lenye utajiri wa mafuta la Bayelsa nchini Nigeria
wameanzisha kampeni maalamu yenye kauli mbiu ya 'sema la kwa waeneza
uvumi'.
Kampeni hiyo imeanzishwa kufuatia kuibuka taharuki baada ya kuenea
uvumi kuwa gavana wa jimbo hilo amefutwa kazi. Katika mabango
yaliyowekwa barabarani Wanigeria wanahimizwa kutosikiliza uvumi wala
kuuhimiza. Wanaoendesha kampeni hiyo wanasema uvumi umeathiri vibaya
utendaji kazi katika jimbo hilo.
Msemaji wa gavana wa jimbo hilo Daniel Iworiso-Markson amewaambia
waandishi habari kuwa kampeni hiyo haina lengo la kuwanyima watu uhuru
wa maoni. Ili kukabiliana na tatizo la uvumi katika jamii, wakuu wa
jimbo hilo wamebuni kamati ya wataalamu watakaowaelimisha watu kuhusu
uovu wa kueneza uvumi. Aidha serikali ya jimbo hilo imetangaza nambari
maalumu za simu ili kila mwenye kutaka habari rasmi azipate kupitia njia
hiyo badala ya kutegemea uvumi. Jimbo la Bayelsa ni nyumbani kwa Rais
Goodluck Jonathan wa Nigeria
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment