Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Thursday, 4 April 2013

Uganda yasitisha operesheni dhidi ya LRA huko CAR


Jeshi la Uganda limetangaza kwamba limesimamisha operesheni zake za kijeshi katika Jamhuri ya Afrika ya Kati kwa lengo la kuwasaka waasi wa kundi la LRA wanaopigana na serikali ya Kampala.
Taarifa ya Jeshi la Uganda imeeleza kuwa, hatua hiyo imechukuliwa baada ya serikali ya nchi hiyo kuangukia mikononi mwa waasi wa Muungano wa Seleka. Jeshi la Uganda limesisitiza kwamba, operesheni ya kumsaka Joseph Kony kiongozi wa kundi la waasi wa LRA, makamanda na wapiganaji wa kundi hilo imesimamishwa hadi hapo baadaye.
Tarehe 23 na 24 ya mwezi uliopita, waasi wa Muungano wa Seleka waliingia mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Bangui na kuipindua serikali ya Rais Francois Bozize kwa madai  ya kukiuka  makubaliano ya amani ya Libreville. Imeelezwa kuwa, Bozize alikimbilia nchini Cameroon na ameomba hifadhi nchini Benin.

0 comments:

Post a Comment