26,Jumaadal ula,1434Hijiriyah/ April 07,2013Miyladiyah
Mbunge
wa Viti maalum Mkoa wa Tanga Amina Mwidau (CUF), kiakabidhi mpira kwa kiongozi
wa timu ya Kata ya Kiomoni, Mohamed Said huku baadhi ya mashabiki wakishuhudia
upokeaji wa mpira huo.
Mbunge
Mwidau, akisalimia na wanawake wa Kata ya Mafuriko, ambao walifika kumlaki
katika ziara yake ya Wilaya ya Tanga
Mbunge
wa viti maalum Mkoa wa Tanga Amina Mwidau (CUF), akipata maelezo ya mradi wa
kisima cha maji kutoka kwa Diwani wa Kata ya Mwera Maisha Mkaidi (CUF), wengine
ni baadhi ya viongozi na wananchi wa kata hiyo.
Mbunge
Mwidau, akikabidhi fedha kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Kipumbwi Jamali Nassoro
kwa ajili ya kununua mifuko kumi ya saruji ikiwa ni sehemu ya ahadi ya mbunge
katika kuunga mkono ujenzi wa shule ya Msingi Kipumbwi Pwani.
Mbunge
Mwidau akikabidhi mifuko kumi ya saruji kwa Ofisa Mtendaji wa Kata ya Msambweni
Bahati Marungu kwa ajili ya ujenzi shule ya Sekondari ya Kata ya Msambweni.
wa yakitokea nchini yamekuwa yakipangwa na kuratibiwa na viongozi wa chama hicho kutimiza ahadi yao ya kuhakikisha nchi haitawaliki.
Mbunge
Mwidau akisalimia na wanawake wa kikundi cha wajasiriamali wafugaji wa kuku wa
Kata ya Pongwe kijiji cha Marizara.
Mbunge
Mwidau, akisalimia na wanawake wa Kata ya Mafuriko, ambao walifika kumlaki
katika ziara yake ya Wilaya ya Tanga
Mbunge
wa viti maalum Mkoa wa Tanga Amina Mwidau (CUF), akipata maelezo ya mradi wa
kisima cha maji kutoka kwa Diwani wa Kata ya Mwera Maisha Mkaidi (CUF), wengine
ni baadhi ya viongozi na wananchi wa kata hiyo.
Mbunge
Mwidau, akikabidhi fedha kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Kipumbwi Jamali Nassoro
kwa ajili ya kununua mifuko kumi ya saruji ikiwa ni sehemu ya ahadi ya mbunge
katika kuunga mkono ujenzi wa shule ya Msingi Kipumbwi Pwani.
Mbunge
Mwidau akikabidhi mifuko kumi ya saruji kwa Ofisa Mtendaji wa Kata ya Msambweni
Bahati Marungu kwa ajili ya ujenzi shule ya Sekondari ya Kata ya Msambweni.
Mbunge
wa Mwidau, akikagua madarasa ya shule ya Sekonadari ya Msambweni, kulia ni
Diwani wa Kata ya Msambweni Abdulrahaman Hassan (CUF).
.....................................................................................
MBUNGE
wa Viti maalum Mkoa wa Tanga, Amina Mwidau (CUF), awametaka wananchi wa mkoa
wake kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo katika
maeneo yao.
Kauli
hiyo aliitoa kwa nyakati tofauti alipokuwa akizungumza katika ziara yake hiyo
katika kata za halmashauri ya jiji la Tanga na Wilaya ya Pangani, ambapo
alisema ni muhimu kwa kila mwanajamii kutambua wajibu wake.
“Suala
la amaendeleo halina itikadi na sasa sio wakati wa kampeni za uchaguzi, ni
jukumu letu kwa viongozi wa Mkoa wa Tanga, kuhakikisha tunashiriki katika
miradi ya maendeleo kwa dhati.
“Ni wazi
Mkoa wa Tanga tuna kila sababu ya kuhakikisha tunaimarisha uchumi wetu hasa
baada ya miaka kadhaa viwanda vyake kufa kutokana na kutokuwepo na usimamizi
mzuri.
Ikiwa kila mtu atatambua wajibu wake ni wazi tutafanikiwa kufikia lengo
letu,” alisema Mwidau.
Alisema
kutokana na hali hiyo kila mara amekuwa akishiriki katika kuhamasisha maendeleo
katika maeneo yote ya mkoa huo bila kujali uongozi wa kaa upo chini ya chama
cha CUF au CCM.
“Tanga
tuna ardhi nzuri na tuna kila sababu ya kujivunia jambo hili ingawa kukosekana kwa usimamizi
madhubuti kwetu imekuwa ni kilio kikubwa kwa wananchi wetu tunaowaongoza, wabunge
wote wa mkoa huu tuna wajibu wa kuliangalia hili,” alisema Mbunge Mwidau.
Katika
ziara hiyo akiwa wilayani Pangani Mwidau, alisema kuwa amefurahishwa kuona
wananchi na viongozi wa Serikali ya Kijiji cha Mwera kuamua kuchimba kisima
kikubwa zaidi ya kilichopo sasa na katika hilo amefurahishwa kuona mchango wa
awali wa mashine aliyoitoa imewezesha kujengwa kwa kisima kisima kingine
kikubwa cha futi 45 na kipenyo cha nchi sita.
"Habari hii ni hisani ya Francis Godwin bloga"
0 comments:
Post a Comment