Imearifiwa kuwa Aprili 8 mwezi huu Jaji Christine Van den Wyngaert raia wa Ubelgiji ameomba kujiondoa kama jaji katika kesi ya Uhuru na Ruto. Kwa mujibu wa tovuti ya ICC, kabla ya kujiondoa Jaji Bi. Wyngaert alishambulia vikali upande wa mashtaka kutokana na usimamizi mbovu wa kesi. Amesema kuna maswali magumu iwapo kweli upande wa mashtaka ulitekeleza uchunguzi kamili dhidi ya washukiwa kabla ya kesi kuanza. Aidha amesema ofisi ya mwendesha mashtaka wa ICC haina kusingizio chochote kuhusu kushindwa kwake kuchunguza iwapo ushahidi uliowasiliwha mbele ya mahakama unaweza kuaminika au la. Mashahidi kadhaa muhimu waliokuwa wamepangwa kutoa ushahidi dhidi ya rais Kenyatta wameshajiondoa. Mwendesha Mashtaka wa ICC anadai kuwa Uhuru, Ruto na mwandishi habari Joshua Sang walihusika katika ghasia za baada ya uchaguzi Kenya mwaka 2007. Hatahivyo wote hao wamekanusha vikali madai hayo ya ICC.
Sikiliza Live
Saturday 27 April 2013
Jaji wa ICC ajiondoa kesi ya Uhuru, Rut
Imearifiwa kuwa Aprili 8 mwezi huu Jaji Christine Van den Wyngaert raia wa Ubelgiji ameomba kujiondoa kama jaji katika kesi ya Uhuru na Ruto. Kwa mujibu wa tovuti ya ICC, kabla ya kujiondoa Jaji Bi. Wyngaert alishambulia vikali upande wa mashtaka kutokana na usimamizi mbovu wa kesi. Amesema kuna maswali magumu iwapo kweli upande wa mashtaka ulitekeleza uchunguzi kamili dhidi ya washukiwa kabla ya kesi kuanza. Aidha amesema ofisi ya mwendesha mashtaka wa ICC haina kusingizio chochote kuhusu kushindwa kwake kuchunguza iwapo ushahidi uliowasiliwha mbele ya mahakama unaweza kuaminika au la. Mashahidi kadhaa muhimu waliokuwa wamepangwa kutoa ushahidi dhidi ya rais Kenyatta wameshajiondoa. Mwendesha Mashtaka wa ICC anadai kuwa Uhuru, Ruto na mwandishi habari Joshua Sang walihusika katika ghasia za baada ya uchaguzi Kenya mwaka 2007. Hatahivyo wote hao wamekanusha vikali madai hayo ya ICC.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment