Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Tuesday 16 April 2013

Israel yatishia kuushambulia Ukanda wa Ghaza



Mkuu wa Jeshi la utawala haramu wa Israel, ametishia kuanzisha mashambulizi mapya dhidi ya Ukanda wa Ghaza. Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa leo na redio ya Israel, Benny Gantz amesema kuwa, vikosi vya utawala wa Kizayuni vinakusudia kuanzisha operesheni kubwa ya kijeshi dhidi ya ukanda huo, kushinda mashambulizi ya siku nane yaliyofanywa na Israel mwishoni mwa mwaka jana. Kuhusiana na uwezekano wa kuanza kwa Itifadha ya Tatu katika maeneo ya Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, Gantz amekiri kuwa, hivi sasa Israel inakabiliwa na changamoto kubwa, tofauti kabisa na changamoto ulizowahi kukabiliana nazo utawala huo wa Kizayuni. Ni vyema kukumbusha hapa kwamba, katika mashambulizi ya siku nane ya Israel dhidi ya Ukanda wa Ghaza, yaliyoanza katikati ya mwezi Novemba mwaka 2012, Wapalestina wasiopungua 190 waliuawa shahidi na maelfu ya wengine kujeruhiwa.

0 comments:

Post a Comment