Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday, 12 January 2013

Njama za Marekani na baadhi ya nchi za Kiarabu za kuiangusha serikali ya Nouri al Maliki

Marekani, ikishirikiana na baadhi ya nchi za eneo ikiwemo Saudi Arabia, Qatar na Uturuki zinajaribu kuzusha machafuko ya ndani nchini Iraq ili kuvuruga amani na uthabiti na kuigawa nchi hiyo. Shirika la habari la Iraq la an Nakhil limeripoti kuwa ghasia zilizotokea katika majuma kadhaa yaliyopita kwenye baadhi ya miji ya Waislamu wa Kisuni nchini humo kama al Anbar, Nainawa na Salahuddin zimechochewa na mirengo yenye mfungamano na madola ya kigeni, kwani viongozi wa Marekani wanatekeleza njama dhidi ya serikali ya Iraq inayoongozwa na Waislamu wa Kishia kwa kuzichochea Saudi Arabia na Qatar dhidi ya serikali hiyo, na sababu ni kwamba Washington inahisi kuendelea kubaki madarakani Waziri Mkuu wa Iraq Nouri al Maliki kunakinzana na maslahi yake katika eneo hili la Mashariki ya Kati.

An Nakhil limeashiria uungaji mkono wa serikali ya Iraq kwa Rais Bashar al Assad wa Syria na kufafanua kuwa maandamano yaliyoratibiwa, ambayo yamefanyika katika maeneo kadhaa ya Iraq chanzo chake ni mitazamo ya serikali ya al Maliki kuhusiana na kadhia ya Syria, na kimsingi ni kwamba kwa kuishinikiza serikali ya Baghdad na kuichochea baadhi ya mirengo ya Iraq dhidi ya serikali hiyo, Saudia, Qatar na Uturuki zimekuwa na nafasi kuu katika ghasia na machafuko yanayoshuhudiwa nchini Iraq.

Wakati huohuo Salman al Musawi, mwanachama wa mrengo wa 'Utawala wa Sheria' katika bunge la Iraq amefichua kuhusika kwa Marekani, Saudi Arabia na Qatar katika maandamano dhidi ya serikali yanayofanyika nchini Iraq na kusisitiza kwamba bunge la nchi hiyo litachukua hatua kuhusiana na nchi zinazochochea ghasia na machafuko nchini humo.

Mbali na wanasiasa, viongozi wa kidini wa Iraq pia wanaamini kuwa ghasia za hivi karibuni nchini humo zimechochewa na madola ya kigeni. Sheikh Mahdi Karbalai, mwakilishi wa Marjaa Mkuu wa Waislamu wa Kishia nchini Iraq Ayatullahil Udhma Sayyid Ali Sistani amezituhumu baadhi ya nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi kuwa zinachochea vurugu ili kuvuruga utulivu na uthabiti nchini Iraq.

Sheikh Mahdi Karbalai, ambaye ni Khatibu wa Sala ya Ijumaa katika mji mtakatifu wa Karbala ametahadharisha juu ya njama za nchi hizo na kuyataka makundi ya kisiasa ya Iraq kutatua matatizo yao ya ndani kwa kuzingatia maslahi ya taifa na kuweka kando matashi ya kikoo na kikaumu. Wakati huohuo katika hatua zinazoendelea kuchukuliwa na serikali ya Waziri Mkuu Nouri al Maliki kwa lengo la kurejesha utulivu kikao cha kwanza cha kamati ya Baraza la Mawaziri ya kufuatilia matakwa ya waandamanaji kimefanyika nchini humo.

Itakumbukwa kuwa mnamo mwezi uliopita wa Desemba na kufuatia kutiwa nguvuni walinzi wa Waziri wa Fedha wa Iraq Rafi'i al Issawi kwa tuhuma za kufanya vitendo vya kigaidi, baadhi ya makundi ya kisiasa nchini humo hususan la Faharasa ya al Iraqiyyah linaloongozwa na Iyad Allawi na kwa uungaji mkono wa Saudi Arabia, Qatar na Uturuki yalichochea maandamano dhidi ya serikali katika baadhi ya miji ya Iraq ya Waislamu wa Kisun

0 comments:

Post a Comment