Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Monday, 22 October 2012

Mwendesha Mashtaka wa ICC awasili Kenya

Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) amewasili nchini Kenya mapema leo na kupokelewa na viongozi wa masuala ya sheria akiwemo Waziri wa Sheria, Eugene Wamalwa. Bi. Fatou Bensouda atakuwa nchini Kenya kwa siku 5 ambapo anatarajiwa kutembelea maeneo yaliyokumbwa na machafuko ya baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007. Pia atatembelea kambi kadhaa za wakimbizi wa ndani pamoja na kukutana na waathiriwa wa ghasia hizo za baada ya uchaguzi. Taarifa kutoka ofisi ya mwanasheria huyo zinasema kuwa lengo la safari yake nchini Kenya ni kujionea kwa karibu athari zilizosababishwa na fujo za kisiasa pamoja na kuandaa mazingira ya kuanza kesi za washukiwa wanne wa ghasia hizo mjini The Hague, Uholanzi mwaka ujao. Ghasia za baada ya uchaguzi mkuu uliopita nchini Kenya zilisababisha vifo vya zaidi ya watu 1400 huku mamia ya maelfu wakilazimika kuyakimbia makazi yao. Wakenya wanne wakiwemo wanasiasa mashuhuri wanatuhumiwa kuhusika na ghasia hizo na kesi zao zinatarajiwa kuanza mwezi Aprili mwakani.

0 comments:

Post a Comment