Sikiliza Live
Monday, 22 October 2012
Kushambulizi Israel meli ya misaada ni uharamia
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema
kwamba, shambulizi lililofanywa na vikosi vya majini vya Israel dhidi
ya meli ya misaada ya kibinadamu kwa ajili ya wakazi wa Gaza ni sawa
kabisa na uharamia na kukiuka wazi haki za binadamu.
Ramin Mehmanparast amesema hayo sambamba na kulaani hatua hiyo ya vikosi
vya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel ya kushambulia meli ya
Estelle iliyokuwa imebebea misaada ya kibinadamu kwa ajili ya wananchi
wa Palestina wa Ukanda wa Gaza wanaoishi katika mzingiro wa utawala huo
ghasibu. Mehmanparast amezitaka mahakama za kimataifa kufuatilia uhalifu
huo na kitendo cha kutekwa nyara wanaharakati wa haki za binadamu na
meli hiyo pamoja na kuchukuliwa hatua za haraka ili kuzuia dhulma
wanayofanyiwa wakazi wa Gaza. Meli hiyo ya Sweden iliyokuwa imebeba
misaada ya kibinadamu kwa ajili ya wakazi wa Gaza ilishambuliwa na jeshi
la Israel Jumamosi iliyopita na kuzuiwa kutia nanga katika pwani ya
Ukanda wa Gaza na hivi sasa inashikiliwa na Israel. Mwaka 2010 katika
tukio kama hilo Israel pia ilishambulia meli ya misaada ya Uturuki
katika maji ya kimataifa na kuwaua wanaharakati 9 na kuwajeruhi wengine
kadhaa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment