Waislamu nchini Tanzania wametoa msimamo juu ya masuala
mbalimbali yanayoendelea nchini wakati wa kongamano lililoandaliwa na
Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee
jijini Dar es Salaam.
Kwenye kongamano hilo ambalo masheikh mbalimbali wakiwemo Sheikh Ponda Issa Ponda, Ally Basaleh, Alhaj Mussa Kundecha na Kondo Juma Bungo waliwasilisha mada mbalimbali pamoja na kutangaza maazimio ya kongamano hilo. Moja ya mambo yaliyozungumzwa ni mapendekezo waliyowasilisha kwenye Tume ya Katiba Mpya ambapo walisema iwapo mapendekezo waliyowasilisha hayatazingatiwa basi Waislamu watatangaza kusimamisha mchakato huo nchi nzima na kufanya maandamano usiku na mchana. Sheikh Ponda amesema kuwa, dhulma na uonevu dhidi ya Waislamu ni mambo ambayo yanayopaswa kukomeshwa nchini humo.
Aidha Sheikh Ponda aliwataka Waislamu wawe na subira hadi utakapokamilika mchakato wa katiba.
Kwenye kongamano hilo ambalo masheikh mbalimbali wakiwemo Sheikh Ponda Issa Ponda, Ally Basaleh, Alhaj Mussa Kundecha na Kondo Juma Bungo waliwasilisha mada mbalimbali pamoja na kutangaza maazimio ya kongamano hilo. Moja ya mambo yaliyozungumzwa ni mapendekezo waliyowasilisha kwenye Tume ya Katiba Mpya ambapo walisema iwapo mapendekezo waliyowasilisha hayatazingatiwa basi Waislamu watatangaza kusimamisha mchakato huo nchi nzima na kufanya maandamano usiku na mchana. Sheikh Ponda amesema kuwa, dhulma na uonevu dhidi ya Waislamu ni mambo ambayo yanayopaswa kukomeshwa nchini humo.
Aidha Sheikh Ponda aliwataka Waislamu wawe na subira hadi utakapokamilika mchakato wa katiba.
0 comments:
Post a Comment