Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Friday 10 May 2013

MGOMO WA DALADALA UMEANZA KWA KASI IRINGA ASUBUHI HII




 Baadhi wananchi wakipanda boda boda maada ya madereva daldal kugoma
Mama na wanawe akiwa juu ya piki piki maarufu kama bodaboda akiwapeleka shule huku askari polisi wakishuhudia usafiri mbadala wa raia manispaa ya Iringa leo asubuhi.
Kazi kweli kweli adha ya usafiri ndiyo hiyo
Baadhi ya abiri wakiwa wamesimama kungojea labda madereva wanaweza kulekeza kamba.
Ama kweli"KUFA KUFAANA"Gari aina CENTER likiwa limepakiza abiria baada ya gari za abilria kugoma kufanya kazi yake.


Mgomo  wa  daladala katika Manispaa ya Iringa umeanza asubuhi hii katika eneo la Mwang'ingo mjini Iringa kwa  madereva na   wamiliki   wa  daladala mjini hapa kudai  kuchoshwa na manyanyaso ya afisa mpya  wa SUMATRA mkoa  wa  Iringa.

Habari  ambazo  mtandao huu  wa  www.francisgodwin.blogspot.com ambazo umezipata zinadai  kuwa hatua ya  mgomo huo  imekuja   kutokana na kuchukizwa  uamuzi  wa Sumatra  mkoa  wa Iringa  kufuta  stendi ya  posta pamoja na  kuzuia daladala  kukaa kwa muda  eneo la stendi ya  daladala  ya Miyomboni maeneo ambayo  kimsingi  walikuwa  wakikaa siku zote. 

Madereva  hao  wamesema  kuwa leo  hawapo   tayari  kufanya kazi hadi  hapo afisa  huyo  wa Sumatra  mkoa  wa Iringa atakapofuta maagizo yake ya  kuzuia stendi hiyo ya  posta na kuruhusu daladala  kukaa muda zaidi  eneo la Miyomboni .
"Picha na habari ni kwa hisani ya Francis Godwin Blogs"

0 comments:

Post a Comment