Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Monday 20 May 2013

Mawaziri watatu kung’olewa madarakani Tanzania

Hali ya mvutano inazidi kushuhudiwa katika chama tawala cha Mapinduzi nhini Tanzania (CCM) ambapo mara hii wabunge wake wamemtaka Rais Jakaya Kikwete kuwafukuza kazi mawaziri watatu serikalini. Mawaziri wanaotakiwa kung’olewa ni pamoja na Dakta Shukuru Kawambwa wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dakta Mathayo David Mathayo wa Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi, na Dakta Fenella Mukangara wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo. Kama Rais Kikwete atakubali kuwafuta kazi mawaziri hao, itakuwa mara ya pili kwake kufanya hivyo ambapo mara ya kwanza ilikuwa mwezi Mei ambapo aliamua kuwaengua madarakani baadhi ya mawaziri waliokuwa wakiandamwa kwa tuhuma mbalimbali, ikiwemo uwajibikaji mbovu na ubadhirifu. Wabunge hao walichukua msimamo huo hapo jana katika kikao baina yao na Rais Kikwete kilichokuwa kikitathimini mwenendo wa chama na utendaji wa wabunge. Wabunge hao walidai kuwa mawaziri hao watatu wamekuwa mzigo kwa Serikali ya CCM kutokana na utendaji wao kutokuwa wa kuridhisha. Walisema matunda ya uwepo wa mawaziri hao kwenye wizara husika hayaonekeni na hivyo kumtaka Rais Kikwete awafute kazi.

0 comments:

Post a Comment