Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Saturday, 12 January 2013

Wanawake Saudia waandamana kudai haki


Wanawake nchini Saudi Arabia wameendeleza maandamano wakitaka kuachiliwa huru wanawake na watoto ambao wanashikiliwa katika jela za nchi hiyo kwa sababu tu ya kuupinga utawala wa kifalme wa Aal Saud.
Katika maandamano ya hivi karibuni, siku ya Jumamosi wanawake waliandamana katika mji wa Buraydah wakidai haki zao na kutaka  wafungwa wa kisiasa waachiliwe huru. Kwa mujibu wa Jumuiya ya Haki za Kisiasa na Kiraia Saudi Arabia, takribani wafungwa 30 elfu wa kisiasa wanashikiliwa katika jela za Ufalme wa Aal Saud. Wafungwa wengi wanashikiliwa gerezani bila kufunguliwa mashtaka huku wengine wakiendelea kuzuiliwa pamoja na kuwa vifungo vyao vimemalizika. Maandamano ya kudai haki hivi karibuni yalifanyika katika mji mtakatifu wa Makkah. Aidha maandamano kama hayo yamekuwa yakifanyika katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo pamoja na mji mkuu Riyadh. Walio wengi Saudi Arabia wanataka uhuru wa kuwachagua viongozi wao pamoja na kukomeshwa dhulma na ubaguzi nchini humo. Maandamano ya wananchi huko Saudia yanafanyika katika fremu ya Mwamko wa Kiislamu ambao umekuwa ukishuhudiwa Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini. Ikumbukwe kuwa Saudi Arabia ni muitifaki mkubwa wa Marekani katika eneo

0 comments:

Post a Comment