Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta mapema leo ametangaza majina zaidi ya watu
 anaowapendekeza kuwa mawaziri kwenye serikali yake mpya. Rais Kenyatta 
amewaarifisha watu 12 wengi wao wakiwa wataalamu. Hata hivyo wanasiasa 
mashuhuri kama vile Najib Balala na Charity Ngilu watapata nafasi ya 
kurudi kwenye baraza la mawaziri iwapo bunge litawaidhinisha. Wawili hao
 ambao wamewahi kuhudumu kama mawaziri katika serikali zilizopita 
wamependekezwa kuongoza wizara za Madini na Ardhi, Nyumba na Maendeleo 
ya miji. Hata hivyo rais wa Kenya bado hajatangaza watu watakaoongoza 
wizara za Mambo ya Ndani na Leba ingawa ameahidi kutoa tangazo kuhusu 
suala hilo katika siku chache zijazo. Wakili mashuhuri na balozi wa 
zamani wa Kenya nchini Ufaransa, Raychelle Omamo anependekezwa kuongoza 
wizara muhimu ya ulinzi. Bi. Omamo anakuwa mwanamke wa kwanza kuwahi 
kushikilia wadhifa huo katika historia ya Kenya.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
 

 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment