Rais Yoweri Museveni wa Uganda amesema ndoto yake kubwa ni kuona bara la
 Afrika likiungana na kuwa kitu kimoja. Rais Museveni amesema nchi za 
Afrika zimeendelea kuwa masikini kutokana na kuwepo ufisadi na 
kukosekana miungano thabiti ya kisiasa na uongozi bora. Amesisitiza 
kuwa, Wakoloni wamefanikiwa kuendeleza ukoloni mamboleo baada ya kumaizi
 kwamba Waafrika hawawezi kujichukulia maamuzi wenyewe bila ya 
kusukumwa. Huku hayo yakijiri, Marais wa nchi za Afrika Mashariki 
wanatarajia kukutana siku ya Jumamosi mjini Arusha, Tanzania ili 
kujadili changamoto zinazoikabili Jumuiya ya EAC. Rais Uhuru Kenyatta wa
 Kenya anatarajiwa kuleta mitazamo mipya na itakuwa mara yake ya kwanza 
kuhudhuria mkutano wa aina hiyo tangu alipoapishwa kuwa rais Aprili 9.
Sikiliza Live
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
 

 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment