Powered by Blogger.

Sikiliza Live

Friday, 11 January 2013

MFALME WA SAUDI ATEUA WANAWAKE KUINGIA BUNGENI

Mfalme Abdullah wa Saudi Arabia, kwa mara ya kwanza ameteua wanawake 30 kuingia katika bunge la nchi hiyo, kwa mujibu wa amri ya kifalme iliyochapishwa na shirika la habari la nchi hiyo SPA. Amri hiyo inawapa wanawake jumla ya  nafasi moja ya tano katika  baraza la Shura, ambalo ndilo bunge rasmi la taifa hilo linaloongoza kwa uzalishaji wa mafuta. Wajumbe wote 150 wa baraza hilo huteuliwa na mfalme. Mwaka 2011 Abdullah aliahidi kuwaruhusu wanawake kugombea na kupiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa kama sehemu ya mageuzi. Uchaguzi ujao utafanyika mwaka 2015. Saudi Arabia ndiyo nchi pekee ya Kiislamu isiyoruhusu wanawake kupiga kura. Wanawake wa Saudi Arabia hawaruhusiwi pia kuendesha magari, na hawawezi kusafiri bila ya kusindikizwa na mlinzi wa kiume au wawe na umri wa zaidi ya miaka 45.

0 comments:

Post a Comment