Sikiliza Live
Friday, 11 January 2013
MAJESHI YA MAREKANI KUACHA MAPIGANO AFGHANISTAN
Rais wa Marekani Barack Obama na mwenzake wa
Afghanistan Hamid Karzai, wamekubaliana kuwa
vikosi vya Marekani nchini Afghanistan vitamaliza
operesheni zake nyingi za mapambano mwishoni
mwa mwaka huu. Viongozi hao walitoa taarifa ya
pamoja katika ikulu ya Marekani White House jana
Ijumaa, kuhusu mustakabali wa vikosi vya Marekani
nchini Afghanistan. Wanajeshi hao wanatarajiwa
kuchukuwa jukumu la usaidizi, miezi michache
mapema kuliko ilivyopangwa. Obama na Karazai pia
waliunga mkono kufanyika kwa mazungumzo mjini
Doha, Qatar, kati ya serikali ya Afghanistan na
viongozi wa kundi la Taliban. Zaidi ya wanajeshi
66,000 wa Marekani walioko Afghanistan
wataondoka mwaka 2014.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

0 comments:
Post a Comment