Sikiliza Live
Friday, 11 January 2013
CAR, WAASI WAFIKIA MAKUBALIANO
Serikali ya Jamhuri ya Afrika ya Kati na waasi
wamekubaliana jana Ijumaa kuunda serikali ya
umoja wa kitaifa, chini ya makubaliano ya kusitisha
mapigano. Makubaliano hayo yaliyosainiwa katika
mji mkuu wa Gabon, Libreville baada ya siku tatu za
upatanishi wa mataifa jirani, yameondoa kitisho
kikubwa zaidi dhidi ya utawala wa muongo mmoja wa
rais Francois Bozize, katika koloni hilo la zamani la
Ufaransa. Msemaji wa muungano wa waasi wa
Seleka Eric Massi alisema makubaliano hayo ni
mazuri kwa mustakabali wa taifa, lakini alionya kuwa
mapigano yanaweza kuripuka tena endapo serikali
itashindwa kutekeleza matakwa ya waasi
yaliyojumlishwa katika makubaliano hayo. Madai
hayo ni pamoja na kuachiwa kwa wafungwa wote wa
kisiasa, na kuondoa vikosi vyote vya kigeni
vilivyoingizwa kusaidiana na serikali. Makubaliano
hayo yalitaka kuundwa kwa serikali ya muungano
ambayo itakuwa na waziri mkuu kutoka upinzani, na
kufanyika kwa uchaguzi wa bunge jipya ndani ya
miezi 12.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

0 comments:
Post a Comment